Mgombea wa urais wa Misri anayetarajiwa
kushinda Abdul Fattah al-Sisi ameapa kuwa atahakikisha kundi la
Muslim Brotherhood lililopigwa marufuku haliwepo tena iwapo atashinda
urais.
Akiongea kwenye mahojiano ya
televisheni al Sisi ambaye alikuwa Mkuu wa Majeshi wa Misri, amesema
majaribio mawili ya kutaka kumuua yalibainika.
Julai mwaka jana Bw. al-Sisi alimuondoa
madarakani rais wa kwanza wa Misri kuchaguliwa kidemokrasia Mohammed
Morsi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni