Kesi iliyopo Mahakama ya Kimataifa ya
Uhalifu (ICC) dhidi ya Naibu Rais wa Kenya William Ruto, itaendelea
mbele licha ya kukabiliwa na vikwazo vikubwa, Mwendesha Mashtaka wa
Mahakama hiyo Fatou Bensouda amesema.
Bensouda pia amesema anapanga kukutana
na katika siku za hivi karibuni na Mwanasheria Mkuu Githu Muigai,
kuzungumzia ombi la mahakama la kutaka kuweza kupata rekodi za
kifedha za Rais Uhuru Kenyatta.
Alipo ulizwa kuhusu kesi ya Ruto,
katika mkutano na waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya Umoja wa
Mataifa, Bi. Bensouda amesema kunavikwazo vingi kwa mashahidi kukataa
kutoa ushahidi baada ya kubadili misimamo yao katika dakika za
mwisho.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni