Jay Z na Rihanna
Imebainika kuwa dada wa Beyoncé,
Solange alimpiga shemeji yake Jay Z katika tukio la kushangaza
lililotokea kwenye lifti baada ya tajiri huyo wa muziki kusema
ataenda kwenye pati ya Rihanna bila ya mkewe Beyoncé.
Kwa mujibu wa New York Daily News,
ugomvi huo ulichochewa na kitendo cha Jay Z, kumcheka Solange wakati
marafiki wake wawili wakingia katika pati katika hoteli ya The
Standard huko Manhattan na kudai ni rafiki wa Jay Z.
Kitendo hicho kilimkera Solange na
kulazimisha yeye, Beyoncé na Jay Z waondoke, ndipo Jay Z aliposema
kuwa yeye anaenda kwenye pati ya Rihanna bila ya mkewe Beyoncé,
jambo lililomkera Solange na kuanza kumpiga.
Beyonce na ndugu yake Solange


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni