Kocha wa timu ya Taifa ya Uholanzi, Louis Van Gaal ameiambia BBC kuwa anataka kuwa kocha mkuu wa klabu ya soka ya Manchester United.
Kocha huyo mwenye miaka 62, amesema anaipenda sana timu hiyo na ana imani atapewa jukumu hilo la kuinoa Manchester, ambayo ni moja ya timu kubwa za soka ulimwenguni.
Kocha huyo anatarajiwa kuchukua mikoba ya David Moyes ambaye alitimuliwa kazi ya kuendelea kuinoa timu hiyo April 22 mwaka huu kutokana na mwenendo mbovu katika ligi kuu ya Uingereza.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni