Zaidi ya wachimba madini 201 wamekufa
na wengine 200 wamekwama chini ya Ardhi baada ya mlipuko wa moto
katika machimbo ya makaa ya mawe katika jimbo la Manisa Magharibi mwa
nchi ya Uturuki.
Waziri wa Wizara ya Nishati nchini humo
Bw. Taner Yildiz amesema watu 787 walikuwa ndani ya mgodi huo wakati
hitilafu ya umeme ilipotokea na kusababisha mlipuko huo.
Ndugu jamaa na Marafiki wa wachimbaji
hao wamekusanyika katika eneo la tukio ambalo ni zaidi ya kilometa
450 kutoka mji mkuu wa nchi hiyo Ankara.
Waokoaji wamefanyakazi usiku mzima
kujaribu kuokoa waliosalia chini ya Ardhi katika ajali hiyo mbaya,
ambapo ni wachimbaji hamsini tu waliookolewa.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni