Wanajeshi nchini Nigeria
wamemfyatulia risasi kamanda wao Kaskazini Mashariki mwa mji wa
Maiduguri.
Meja Jenerali Ahmed Mohammed
amefanikiwa kutoka salama katika tukio hilo kwenye gari lake wakati
wanajeshi hao walipolifyatulia risasi katika kambi ya Maimalari.
Wanajeshi hao wanamtuhumu kamanda
huyo kwa kumuua mwenzao katika shambulio la wapiganaji wanaohisiwa
kuwa ni wa Boko Haram.
Wakati huo huo Rais wa Nigeria
amekanusha kuwaachia huru wafungwa wa kundi la Boko Haram ili
kubadilishana na wanafunzi wasichana zaidi ya 200 waliotekwa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni