.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 12 Juni 2014

UTAWALA WA KIJESHI WAAGIZA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA KUONYESHWA BURE

Utawala wa Jeshi wa nchi ya Thailand umeagiza Wamiliki wa Vituo vya Televisheni kuhakikisha kuwa mashabiki soka nchini humo hawalipi fedha ili kuona michezo ya Kombe la Dunia inayoanza leo nchini Brazil.

Jeshi limesema uamuzi huo ni sehemu ya kampeni ya furaha kwa wananchi wa nchi hiyo kampeni ambayo imekuwa ikitoa huduma za bure za kukata nywele na uwepo wa matamasha ya muziki ya bure.

Mmiliki wa Kituo Televisheni kilichonunua haki za kuonyesha michuano ya Kombe la Dunia amedai kutaka kulipwa fidia ya dola milioni 21.5, kutokana na uamuzi huo wa jeshi la Thailand kutaka michuano ya kombe la dunia kuonyeshwa bure.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni