Mwanasoka Cristiano Ronaldo akiwa benchi ameshuhudia Real Madrid ikipoteza mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Roma jana usiku kwa kukubali kipigo cha bao 1-0.
Bao la Francesco Totti lililofungwa
katika kipindi cha pili lilitosha kabisa kukizima kikosi cha Carlo
Ancelotti kilichokosa makali ya ufungaji.
Mchezo huo ulibidi usimame kwa muda
baada ya baadhi ya mashabiki kuvamia uwanjani ili kuwakaribia
wachezaji wanaowapenda kuwakumbatia, kusalimiana nao na hata kupiga
nao picha kwa kutumia simu zao.
Shabiki akipiga picha na Isco
Shabiki akidhibitiwa na askari





Hakuna maoni :
Chapisha Maoni