.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 30 Julai 2014

MAN UTD YAIFUNGA INTER MILAN KWA MATUTA 5-3 JIJINI WASHINGTON DC

Kocha Louis van Gaal ameendelea kuinoa vyema Manchester United baada ya kupata ushindi mwingine wa penati 5-3 dhidi ya Inter Milan katika mchezo wa kujiandaa na ligi kuu ya Uingereza uliochezwa jana Jijini Washington DC.

Katika mchezo huo ulioisha kwa sare tasa ya 0-0, magoli ya penati ya Manchester United yalipachikwa kimaini na Ashley Young, Javier Hernandez, Tom Cleverley, Shinji Kagawa na Darren Fletcher.

Manchester United kwa sasa imeshinda michezo yake yote mitatu ya kirafiki katika ziara yake hiyo ya nchini Marekani.
Kocha van Gaal  na Ryan Giggs wakifurahia mchezo huo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni