.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 30 Julai 2014

KIFARU CHA ISAREL CHATUPA KOMBORA KATIKA SHULE YA UMOJA WA MATAIFA INAYOHIFADHI WAKIMBIZI HUKO GAZA

Umoja wa Mataifa umesema kombora lililorushwa na kifaru limeuwa wapalestina 15 waliokuwa wamehifadhiwa kwenye shule moja inayohifadhi wakimbizi huko Gaza.

Mashahidi katika shule hiyo ya Abu Hussein inayosimamiwa na Umoja wa Mataifa ambapo maelfu wamekimbilia kujihifadhi, wamesema kuta zimeteketezwa na kombora hilo.

Israeli ambayo imekuwa ikilituhumu kundi la Hamas kutumia shule kama kambi zake za kurushia makombora ya roketi, imesema itachunguza tukio hilo.

Hadi sasa Wapalestina wapatao 1,200 na Waisraeli 55 wameuwawa tangu kuanza kwa mapigano Julai 8, mwaka huu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni