Jaji mmoja nchini Marekani,
amewashangaza wengi baada kuonekana kutomfahamu kabisa mwanamuziki
nyota Rihanna, baada ya kuuliza mahakamani hivi huyo Rihanna ni
nani?.
Inaonekana umaarufu wa Rihanna
uliotokana na kuuza nakala za albam milioni 30 duniani si kitu, baada
ya Jaji huyo kuletewa kesi ya mtu anayetuhumiwa kufuatilia nyendo na
maisha ya Rihanna na Jaji huyo kushindwa kumtambua Rihanna.
Baada ya Jaji Abraham Clott kuambia
mtu asiyenamakazi maalum, Kevin McGlynn amekamatwa kwa kosa la
kufuatilia nyendo na maisha ya Rihanna, Jaji huyo alisema hafahamu
kabisa huyo Rihanna ni nani.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni