.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 27 Julai 2014

KENYA YAPATA MEDALI YA KWANZA YA DHAHABU JUMUIYA YA MADOLA

Kenya imepata medali yake ya dhahabu ya kwanza katika michuano ya Jumuiaya ya Madola baada ya Flomena Daniel kumuongoza mwenzake Caroline Kilel kumaliza mbio za marathoni wanawake huku Kenya ikishika nafasi ya kwanza na ya pili hii leo.

Flomena ambaye ni mshindi wa mbio za marathoni za Paris amemaliza mbio hizo kwa kutumia muda wa saa 2 dakika 26 na sekunde 45, huku Kilel.

Muastralia Jess Trengrove alichuana vikali na kuchukua nafasi ya tatu, na kumshinda kasi Mnamibia Helalia Johannes.na kutwa medali ya shaba.

Katika mbio za wanaume Muaustralia Michael Shelley aliwashangaza wengi kwa kuongoza mbio za kilomita 8, ambazo huwa zinatwaliwa na wakimbiaji wa Afrika na kufanikiwa kutwaa medali ya dhahabu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni