Josephine Kulea akisikiliza hotuba
ya rais Barack Obama katika mkutano Jijini Washington DC.
Rais Barack Obama amesema Marekani
itaanzisha kituo cha uongozi nchini Kenya ili kuwafundisha vijana wa
Afrika Mashariki kumudu kushika nafasi za uongozi kwenye Biashara,
Serikali pamoja na katika Asasi za kiraia.
Rais Obama amebainisha jitihada hizo
katika hotuba yake aliyoitoa kwenye mkutano wa Jitihada za Vijana wa
Afrika Viongozi uliofanyika Jijini Washington DC na kuhudhuriwa na
vijana wapatoa 450 kutoka nchi mbalimbali za Afrika.
Mbali na Kenya Rais Obama amesema
vituo vingine vya kikanda vya kuwajenga viongozi vijana wa Afrika
vitafunguliwa katika nchi za Senegal, Ghana pamoja na Afrika Kusini.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni