Maafisa wa Marekani wamesema moto
unaosambaa kwa kasi huko California umeteketeza nyumba 10 na
kulazimisha mamia ya watu kuhamishwa.
Katika mkoa wa Sacramento moto
umesambaa katika eneo la ekari 4,000, huku moto mwingine unatishia
kuteketeza nyumba karibu na mbuga ya taifa ya Yosemite.
Katika tukio lingine mtu aliye na
umri wa miaka 20 amekufa na wengine wamejeruhiwa kwa radi iliyotokana
na mvua isiyoyakawaida wakati huu wa msimu wa joto huko Los Angeles.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni