Polisi nchini Kenya wanachunguza
mazingira ambayo mwanaume mmoja aliyekuwa akishikiliwa na polisi kwa
deni la shilingi 600 za Kenya kufiwa kizuizini.
Polisi wanajaribu kubaini kwa namna
gani mwanaume huyo Fredrick Mbura aliishia kushikiliwa na polisi
kutokana na deni hilo.
Marehemu Mbura aliswekwa rumande na
polisi wa kituo cha Kasarani siku ya Ijumaa kutokana na deni hilo
analodaiwa na duka la Nawa Auto Spares ambapo alishakuwa ameshalipa
sh 3000 za Kenya na kubaki 600 kumaliza deni.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni