Watu 48 wamefariki dunia baada ya
ndege ya abiria kuanguka nchini Taiwan eneo la Penghu archipelago
kufuatia hali mbaya ya hewa iliyosababishwa na mvua kubwa.
Ndege hiyo iliyokuwa imebeba abiria
58 imeanguka juu ya majengo baada ya kushindwa kutua kwenye uwanja wa
ndege wa Magong.
Watu kumi tu waliokuwa kwenye ndege
hiyo ndio wamenusurika kifo ambapo wamejeruhiwa na kukimbizwa
hospitali.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni