Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar
es Salaam linawashikilia watu wanane kwa kuhusika na tukio la kutupa
mabaki ya miili ya binadamu katika msitu mdogo uliopo eneo la Mpiji,
Kata ya Mbweni, Wilaya ya Kinondoni.
Akiongea leo Kamanda wa Kanda Maalum
ya Dar es Salaam Suleiman Kova, amesema miongoni mwa watu
waliokamatwa wamo pia madaktari wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba
na Teknolojia (IMTU), ambapo miili hiyo ilikuwa imehifadhiwa kwa
ajili ya mafunzo.
Kamanda Kova amesema kuwa jeshi la
polisi limeunda jopo la watu saba la maafisa wa upelelezi
linaloongozwa na Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
Jafari Mohamed ili kubaini sababu zilizopelekea Chuo cha IMTU kutupa
viungo hivyo vya Binadamu maeneo hayo.
Aidha, Kamanda Kova amesema jeshi la
polisi pia litawahusisha Mkemia Mkuu wa Serikali na Mwanasheria Mkuu
ili kubaini miili hiyo ni ya kina nani ilipatikana vipi na kwa kibali
gani ikiwa ni pamoja na kufahamu hatua za kisheria zitatumika
kuwaadhibu wahusika.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni