Mfululizo wa milipuko ya gesi kusini
mwa Taiwan katika mji wa Kaohsiung imeuwa watu 24 na kujeruhi watu
270.
Milipuko hiyo imetikisa wilaya ya
mji huo ya Cianjhen, magari yaliyorushwa yamesambaa na
barabara zimepasuka na kuwa na mitaro.
Chanzo halisi cha kuvuja kwa gasi
hakijafahamika, lakini imefahamika kuwa milipuko hiyo imetokana na
kupasuka kwa mabomba ya gesi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni