Kapteni wa Harambee Stars Victor
Wanyama ameokolewa kutoka kwa kundi la mashabiki wenye hasira Jijini
Nairobi baada ya Harambee Stars kutolewa nje ya michuano ya kuwania
kufuzu kutinga michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika na timu ndogo
ya Lesotho.
Kiungo huyo wa timu ya Southampton
ilibidi atolewe uwanjani na kukimbizwa sehemu salama na polisi wa
Kenya, baada ya Harambee Stars kudhibitiwa na kutoka sare tasa, na
kuifanya Lesotho kusonga mbele kwa ushindi wa awali wa bao 1 bila
walioupata nyumbani.
Mara baada ya matokeo hayo Kenya
ilimtimua kazi kocha Adel Amrouche, raia wa Ubelgiji mwenye asili ya
Algeria, kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la Kenya.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni