.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 4 Agosti 2014

UINGEREZA YASEMA ABIRIA MWANAMKE TOKA SIERRA LEONE HAKUFA KWA EBOLA

Hofu ilitanda kwa muda nchini Uingereza ya kuwepo kwa ugonjwa wa Ebola, baada ya abiria mmoja mwanamke mwenye miaka 72 kufariki dunia muda mfupi tu baada ya kutua nchini humo. 

Mwanamke huyo raia wa Sierra Leone aliyesafiri na ndege ya shirika la ndege la Gambia, alitapika sana na kutokwa na jasho jingi sana alipofika katika uwanja wa ndege wa Gatwick, na alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa hospital. 

Hata hivyo vipimo baadaye vilionyesha mwanamke huyo hakufariki kwa ugonjwa wa Ebola ambao tayari umeshaua zaidi ya watu 256 nchini Sierra Leone.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni