Tanzania Creative Industries
Network (TACIN) kwa kushirikiana na TPDC wanakuletea Tamasha kubwa la Mtwara
Festival katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Mjini Mtwara kuanzia 16 hadi 17 mwezi huu wa nane mwaka 2014.
Mtwara Festival ni jukwaa
endelevu la kuwaleta pamoja wana Mtwara na Lindi wakifurahia tamaduni zao, huku
wakihamasihwa na kupata taarifa juu ya fursa mbali mbali za ajira na kipato
zinazotokana na uwekezaji unaoongezeka kwa kasi kubwa.
Kauli Mbiu ni “Fursa
zimefunguka, Tuzitambue, Tujiandae na Tuzichangamkie “.
Mtwara Festival 2014 itakuwa
ni mchanganyiko wa burudani na utalii, na pia itakuwa na fursa kwa wafanyabiashara pamoja na
sekta binafsi kutangaza biashara na huduma zao.
Ili kushiriki tamasha hili
la aina yake, wasilisha maombi yako sasa kupitia namba za simu, 0754 280 491 au
0784 280 491.
Mtwara Festival 2014, Imedhaminiwa
na TPDC, PSPF, Tanzania Distilleries Ltd, Air Tanzania na PPF.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni