Maafisa wa Wizara ya Afya ya wa
Uganda wamemuweka mtu mmoja anayeshukiwa kuugua ugonjwa wa Ebola
katika chumba cha pekee yake katika hospitali ya Daraja B ya Entebbe.
Mkurugenzi Mkuu Huduma za Afya
katika wizara hiyo, Dk. Jane Aceng, amesema mtu huyo ambaye ni
mtumishi wa afya alibainika kuwa na ugonjwa huo alipofanyiwa vipimo
katika uwanja wa Entebbe wakati alipowasili.
Mgonjwa huyo alikuwa anafanya kazi
na shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa, Sudani Kusini, ambapo
aliletwa Kampala kwa ajili ya matibabu ya homa ya inni, lakini
imebainika kuwa huenda ni Ebola.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni