Nchi ya Guinea imefunga mipaka yake
na Liberia pamoja na Sierra Leone katika kudhibiti kusambaa kwa
ugonjwa hatari wa Ebola uliokwisha uwa watu 959 katika nchi hizo
tatu.
Mlipuko huo wa sasa wa Ebola
inaaminika ulianzia Guinea, hata hivyo Liberia na Sierra leone ndizo
kwa sasa zinakabiliwa na kasi kubwa ya maambukizi mapya ya virusi vya
Ebola.
Shirika la Afya Duniani (WHO) Ijumaa
lilitangaza kuwa kusambaa kwa virusi vya ugonjwa huo ni janga la afya
la dharura.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni