.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 10 Agosti 2014

WAKURD WAWAOKOA WATU WALIOZINGIRWA NA WAPIGANAJI WA KIISLAM NCHINI IRAK

Mamia ya wakimbizi wa kabila la Yazidi nchini Irak waliokwama kwenye milima wakiwa wamezingirwa pande zote na kundi la Waislamu wenye msimamo mkali wanaotaka kuanzisha taifa la Kiislam, wamesindikizwa katika sehemu salama.

Wapiganaji wa Kikurd wa kikosi cha peshmerga wametumia matrekta, malori pamoja na punda kuwaondoa katika eneo hilo, baada ya kukosa misaada kutokana na vikosi vya Marekani kuendelea kuwashambulia kwa anga wapiganaji wa Kiislam.

Baadhi ya watu wa kundi hilo la kabila ndogo la Yazidi, walilazimika kuondolewa eneo hilo kwa miguu, wakipitia kwenye jangwa, ambapo inaaminika karibu watu 5,000 walipelekwa mahala salama na wapiganaji wa Kikurd. Bado kuna maelfu yao wapo katika maeneo hatari kwenye mlima Sinjar.
     Mama akiwa juu ya punda akiondolewa eneo hatari na wapiganaji Wakikurd
 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni