.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 3 Agosti 2014

NYOTA WA MPIRA WA KIKAPU WA MAREKANI AVUNJIKA MGUU MAZOEZINI

Nyota wa Mpira wa Kikapu wa Indiana Pacers Paul George amepoteza matumaini ya kucheza Michuano ya Kombe la Dunia, baada ya kuvunjika mguu wakati wa mazoezi ya timu ya taifa ya Marekani huko Las Vegas.

George ambaye ameshakua mchezaji bora mara mbili wa Ligi Kuu ya Kikapu ya NBA, alikuwa akifanya mazoezi na kikosi mchanganyiko cha Marekani, alipoumia vibaya na kuvunjika mguu wakati akitua kwa nyuma.

Baada ya tukio hilo George ilibidi abebwe kwa machela na kutolewa uwanjani huku wachezaji wenzake wa Marekani wakimuangalia kwa mshtuko kufuatia tukio hilo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni