Watu wapatao 150
wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya tetemeko la ardhi
lenye kipimo cha 6.1 kulikumba eneo la kusini magharibi mwa China hii
leo.
Wataalamu wa
Masula ya Miamba wa Marekani wamesema tetemeko hilo limelikumba eneo
la kilomita 11 kaskazini magharibi mwa mkoa wa Wenping Yuannan majira
ya saa kumi na nusu saa za huko.
Mmoja wa maafisa
wa eneo hilo ameliambia shirika la habari la china la Xinhua kuwa
nyumba nyingi zimeporomoka.
Shirika la
Utangazaji la taifa la China la CCTV, limesema kuwa tetemeko hilo ni
kubwa kuwahi kutokea katika mkoa huo tangu miaka 14 kupita.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni