.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 8 Agosti 2014

RAIS OBAMA AAMURU KUFANYWA MASHAMBULIZI YA ANGA NCHINI IRAK

Rais Barack Obama ameamuru kutekelezwa kwa mashambulizia ya anga dhidi ya wapiganaji wa Kiislam wa Kaskazini mwa Irak, hata hivyo amesema hatorudisha majeshi ya Marekani nchini humo.

Amesema wapiganaji wa Dola ya Kiislam (IS), watalengwa katika mashambulizi hayo ili kudhiditi vitendo vya mauaji vinavyofanywa dhidi ya watu wa madhehebu mengine madogo, na kuhatarisha masilahi ya Marekani.

Mashambulizi hayo ya anga hayajaanza, hata hivyo Marekani imekuwa ikidondosha misaada ya kibinadamu kwa njia ya ndege kutokana na tishio la wapiganaji hao.

IS wametwaa mji mkubwa wanaoishi Wakristo nchini Irak wa Qaraqosh, na kuwafanya wakazi wake kuukimbia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni