Kesi ya mauaji ya mwanamitindo Reeva
Steenkamp inayomkabili mwanariadha mlemavu,Oscar Pistorius wa Afrika
Kusini, imeendelea leo ambapo upande wa utetezi umewasilisha utetezi
wao wa mwisho.
Wakili Barry Roux na timu yake ya
utetezi, katika maelezo yao wamewalaumu polisi kwa kuvuruga ushahidi
muhimu katika eneo la tukio na hivyo kufanya ushahidi uliotokana na
eneo la tukio kuwa si halali.
Upande huu wa utetezi umetumia muda
wake wa kukamilisha hoja zao katika kesi hiyyo kwa kuuhumu upande wa
mashtaka kwa kesi hii kwa makosa ya udanganyifu na kuharibu ushahidi.
Wakili Barry Roux amesema
mwanariadha huyo mlemavu aliyekatwa miguu yake miwili, anapaswa
kukabiliwa na shtaka la kuua bila ya kukusudia, na si kesi ya mauaji
ya mpenzi wakeReeva Steenkamp.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni