Shirika la Afya Duniani (WHO)
limetangaza kusambaa kwa ugonjwa hatari wa Ebola katika nchi za
Afrika ya Magharibi kuwa ni janga la afya la dharura.
Maafisa wa shirika hilo wamesema
kunauwezekani maafa ya ugonjwa huo yakawa makubwa kutokana kusambaa
kwa virusi vya ugonjwa huo.
Tangazo hilo limetolewa baada ya
mkutano wa dharura wa siku mbili huko Switzerland kujadili ugonjwa
huo uliosababisha vifo vya watu 930 katika nchi za Afrika ya
Magharibi katika mwaka huu.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni