Zoezi la kuandikisha watumishi wote
wa umma nchini Kenya pamoja na wa serekali za kaunti kwa kutumia
tekinolojia ya mfumo wa biometric, litaanza kesho nchini humo majira
ya saa tatu asubuhi.
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta
atazindua rasmi zoezi hilo na Naibu Rais wake William Ruto pamoja na
Gavana wa Nairobi Dk. Evans Kidero wakiwa kwenye ofisi zao kila
mmoja.
Waziri wa Mgawanyo wa Madaraka na
Mipango nchini Kenya Bi. Anne Waiguru amesema ofisi yake
imewaandikiwa mawaziri wote kushiriki zoezi hilo la kujiandikisha kwa
kutumia mfumo huo wa kielektroniki.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni