Marekani imesema imefanya operesheni
za kijeshi dhidi ya kundi la kigaidi la al-Shabaab nchini Somalia .
Msemaji wa Pentagon amesema kwa sasa
wanafanya tathimini ya operesheni hiyo iliyofanyika jana kabla ya
kutoa taarifa zaidi.
Hata hivyo maafisa wa Marekani
wanenukuliwa na vyombo vya Marekani wakisema operesheni hiyo
ilimlenga kiongozi wa juu wa al-Shabaab.
Kundi hilo lenye uhusiano na la
al-Qaeda lilipoteza umiliki wa Mogadishu kwa vikosi vya Umoja wa
Afrika mwaka 2011, lakini bado linashikilia maeneo ya kusini na ya
kati ya Somalia.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni