.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 22 Oktoba 2014

DAKTARI WA DRC ASHINDA TUZO ULAYA, KWA KUWASADIA WANAWAKE WALIOBAKWA

Daktari wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ameshinda tuzo ya juu ya Haki za Binadamu Ulaya kwa kuwasaidia maelfu ya waathirika wa matukio ya kubakwa na watu wengi nchini kwake.

Daktari huyo Denis Mukwege alitangazwa mshindi wa tuzo hiyo ya Sakharov na bunge la Ulaya huko Strasbourg, ambayo inaendana na zawadi ya dola elfu 63.

Daktari huyo wa wanawake alianzisha Hospitali ya Pazi, mashariki mwa Congo mwaka 1999 ili kuwatibu wanawake ambao wamekumbwa na matukio ya kutisha ya kubakwa.

Miaka miwili iliyopita Dk. Mukwege alinusurika kuuwawa kwa kutuhumu kuendelea kwa ukatili wa kingono nchini DRC unaofanywa na vikosi vinavyopigana kumiliki eneo lenye utajiri wa madini.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni