Idara ya Ulinzi ya Marekani imesema
inachunguza video ya wapiganaji wa Dola ya Kiislama (IS)
inayoonyesha wapiganaji wa kundi hilo wakiwa na silaha za Marekani
zilizodondoshwa kwa ndege kwa ajili ya wapiganaji wa Kikurdi.
Jumla ya vifurushi 27 vikiwa na
silaha ndogo za kivita, risasi pamoja na vifaa vingine vya kivita
vilidondoshwa Jumatatu, ili kuwasaidia wakurdi kuulinda mji wa Kobane
dhidi ya IS.
Msemaji wa Pentagon amesema idadi
kubwa ya silaha hizo zimewafikiwa walengwa na zipo katika mikono
salama.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni