Katibu Mkuu wa Shirika la Msalaba
Mwekundu Kenya Bw. Abbas Gullet
Chama cha Msalaba Mwekundu Kenya,
kitawasafirisha kwa ndege kutoka Liberia raia 12 wa Kenya waliokwama
katika nchi hiyo iliyokumbwa na mlipuko wa Ebola.
Shirika hilo la Misaada ya
Kibinadamu litawanunulia tiketi za ndege wakenya hao na baadae
kupeleka madai yao Wizara ya Mambo ya Nje.
Makubaliano hayo yamefikiwa jana
baada suala hilo kuingiliwa kati na baadhi ya wakenya wanaofanya kazi
katika Mashiriki ya Kimataifa nchini Liberia.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni