.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 19 Oktoba 2014

KOCHA JOSE MOURINHO AJIGAMBA KUWA CHELSEA INAWEZA KUTWAA TAJI LA LIGI YA NCHI YOYOTE

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amejitapa kuwa Chelsea itashinda taji katika ligi ya nchi yoyote kutokana na kiwango ilichonacho timu hiyo hivi sasa.

Mourinho ambaye kwa sasa timu yake inaongoza Ligi Kuu ya Uingereza kwa tofauti ya pointi tano ametoa majigambo hayo baada ya jana kuifunga Crystal Palace mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la Selhurst Park.

Hata hivyo Kocha wa Crystal Palace, Neil Warnock amesema refa aliyechezesha mchezo huo Craig Pawson alishawishika na vitendo vya wachezaji wa Chelsea na kupelekea kumpa kadi nyekundu mchezaji wake Damien Delaney.
 
Oscar akifurahia goli

Nayo timu ya Manchester City iliitundika Tottenham mabao 4-1 huku  Muargentina Sergio Aguero akipachika mabao yote manne.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni