.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 22 Oktoba 2014

MVUA KUBWA YAANGUSHA NYUMBA 46 NA KUZIFANYA FAMILIA 215 KUKOSA MAKAZI

Mvua kubwa iliyonyesha kwa saa nane katika kijiji cha Nyamikoma kata ya Kabita wilayani Busega, imesababisha watu 215 kukosa makazi huku nyumba 46 zikianguka.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake waliothirika na mvua hiyo, Paul Mchele, amesema familia yake ya watu 11 kwa sasa haina pa kuishi baada ya mvua hiyo iliyoanza saa 10.45 alfajiri na kukatika saa 6 mchana kusomba kila kitu.

Mtendaji wa kijiji hicho, Juma Msema, amesema mvua hiyo imesababisha majanga makubwa kutokana na mvua hiyo kusababisha mafuriko lakini anashukuru kwa kutoripotiwa kifo cha aina yoyote ingawa wananchi wamepoteza mali zao.

Mkuu wa wilaya hiyo, Paul Mzindakaya, ameiagiza kamati ya maafa kufanya tathimini ya haraka ili kuwasaidia waathjirika hao.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni