.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 22 Oktoba 2014

UNGA WA MUHOGO WAUWA WATU WAWILI WA FAMILIA MOJA MKOANI KAGERA

Watu wawili wa familia moja wamefariki dunia baada ya kula chakula kinachosadikiwa kuwa na sumu katika kijiji cha Miranda tarafa ya Nshamba wilayani Muleba, huku watoto wengine wanne wakiwa hospitalini wakipatiwa matibabu.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera, Henry Mwaibambe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja waliopoteza maisha kwa madai ya kula ugali wa muhogo ni Oliva Wilson miaka 42 na Nemilius Wilson miaka mitano.

Amesema watoto wengine wanne wa mama huyo Avira Wilson miaka 10, Frolida na Frola Wilson mapacha wenye miaka saba na Scarion Wilson miaka miwili, wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Rubya.

Kamanda Mwaibambe amesema unga wanaosadikiwa kuutumiwa kwa ugali watu hao, umekusanywa na kupelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali kwa ajili ya vipimo ili kubaini kama ulikuwa na sumu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni