.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 19 Oktoba 2014

WANAHARAKATI WA MASHOGA WA KANISA KATOLIKI WAKERWA NA UAMUZI WA MAASKOFU

Kundi la Kanisa Katoliki linalotetea haki za mashoga, limekerwa na uamuzi wa maaskofu kupinga wito wa kanisa hilo kuwakubali mashoga, wito ambao unaungwa mkono na Papa Francis.

Rasimu ya ripoti hiyo ambayo pia ilikuwa inalitaka kanisa kuwavumilia wanandoa waliotengana na kuoa tena, ilishindwa kupata theluthi mbili ya maaskofu wanayoiunga mkono katika Sinodi huko Roma.

Ripoti rasmi ya mwisho imeeleza kuwa suala pekee litakalofanywa ni kwa wanaopinga mashoga kujiepusha na kuwanyanyapaa mashoga.

Papa Francis ameagiza ripoti hiyo yote, ikiwemo mapendekezo yaliyokataliwa kuchapishwa. Sinodi ya Maskofu wa Kanisa Katoliki watakutana tena mwakani.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni