.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 14 Oktoba 2014

ZOEZI LA UOPOAJI WA MIILI KATIKA AJALI YA MITUMBWI ZIWA TANGANYIKA LASITISHWA

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma,Kanali mstaafu Issa Machibya akiongea na waandishi wa habari(ambao hawapo pichani)ofisini kwake juu ya kusitisha kwa zoezi la uopoaji wa miili ya ajali ya mitumbwi iliyotokea hivi karibuni katika kijiji cha kalalangabo ziwa Tanganyika.

Na Editha Karlo wa blog ya jamii,Kigoma

Serekali ya Mkoa wa Kigoma imesitisha zoezi la uopoaji wa miili ya ajali ya mitumbwi miwili ya maharusi iliyotokea tokea hivi karibuni katika Ziwa Tanganyika kwenye kijiji cha Kalalangabo kilichopo mwambao mwa ziwa Tanganyika .

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali Mstaafu Issa Machibya alisema kuwa vikosi mbalimbali vya ukoaji kwa kushirikiana jeshi la wananchi(JWTZ)wakishirikiana na wananchi wamefanya kazi kubwa sana ya kuopoa miili kwa kipindi cha siku tatu mfululizo.

Amesema jumla ya miili kumi ili patikana katika zoezi hilo la ukoaji lakini hivi sasa wameachia uongozi wa kijiji cha serekali ya kalalangabo kuendelea kutoa taarifa kama kuna miili mingine itakayoibuka kutokana na kuhofiwa kuwa bado miili mingi ipo majini


Mkuu wa Mkoa aliwataka wananchi kuacha tabia ya kutumia vyombo visivyo rasmi katika usafiri na ambavyo havijasajiliwa na mamlaka ya usafiri wa nchi kavu na majini (SUMATRA)pia aliwataka wavuvi na wale wenye vyombo majini waache tabia ya kusafirisha abiria kwa kutumia mitumbwi ya kuvulia dagaa ili kuepuka ajali.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni