.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 30 Novemba 2014

AFISA WA REBUPLICAN AOMBA RADHI BAADA YA KUWASHUTUMU MABINTI WA RAIS OBAMA

Mabinti wa Rais Barack Obama, Sasha na Malia wametuhumiwa kuonyesha kutokuwa na heshima na hawana viwango na afisa mmoja wa chama cha Republican baada ya kuonekana katika hafla ya sherehe za Thanksgiving wakiwa wamevalia vimini.

Afisa huyo Elizabeth Lauten, ambaye ni mkurugenzi wa mawasiliano wa mjumbe wa Baraza la Congress Stephen Fincher, aliandika hayo kupitia ukurasa wake wa Facebook, na kisha kufuta, baada ya kushambuliwa mno kwa kutoa maneono yenye kuumiza, ambapo pia ameomba msamaha.

Lauten aliwatuhumu pia mabinti hao wa rais Obama, walionekana wakiwa wameboreka wakati wakiwa wamesimama pamoja na baba yao, katika kitendo cha utumaduni wa Ikulu kuwaachia huru batamzinga wawili ili kuwaepusha kutumika kama mlo wa jioni wakati wa sherehe za Thanksgiving.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni