Mwanasoka veterani wa
Uingereza David Beckham amepata ajali ya gari leo asubuhi wakati
akienda kumchukua mtoto wake Brooklyn katika uwanja wa mazoezi ya
mpira vya klabu ya timu ya Arsenal.
Beckham, 39, alikuwa
katika uwanja huo wa mazoezi wa London Colney, Hertfordshire,
akimuangalia mtoto waki huyo mkubwa wa kiume Brooklyn, 15, akichezea
timu hiyo ya wachezaji chini ya miaka 16 dhidi ya Brighton.
Hata hivyo katika ajali
hiyo kapteni huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza na mwanae
Brooklyn hawakupata majeraha yoyote, licha ya gari lao kuharibika na
kulazimika kutumia gari lingine.
David Beckham akiwa na
watoto wake wa liume Brooklyn (kushoto), Cruz (katikati) na Romeo
(kulia).


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni