.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 30 Novemba 2014

DAVID BECKHAM APATA AJALI NA MWANAE AKITOKEA KWENYE DIMBA LA ARSENAL

                                              Brooklyn akiwa na baba yake David Beckham

Mwanasoka veterani wa Uingereza David Beckham amepata ajali ya gari leo asubuhi wakati akienda kumchukua mtoto wake Brooklyn katika uwanja wa mazoezi ya mpira vya klabu ya timu ya Arsenal.

Beckham, 39, alikuwa katika uwanja huo wa mazoezi wa London Colney, Hertfordshire, akimuangalia mtoto waki huyo mkubwa wa kiume Brooklyn, 15, akichezea timu hiyo ya wachezaji chini ya miaka 16 dhidi ya Brighton.

Hata hivyo katika ajali hiyo kapteni huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza na mwanae Brooklyn hawakupata majeraha yoyote, licha ya gari lao kuharibika na kulazimika kutumia gari lingine.
David Beckham akiwa na watoto wake wa liume Brooklyn (kushoto), Cruz (katikati) na Romeo (kulia).

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni