.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 30 Novemba 2014

BONDIA TYSON FURY AMDUNDA DERECK CHISORA NA KUTWAA MIKANDA MIWILI

Bondia Tyson Fury ameshinda mataji mawili ya mkanda wa uzito wa juu wa Uingereza na Ulaya, katika raundi ya 10 kwenye pambano lake na bondia aliyesalimu amri Dereck Chisora kwenye ukumbi wa ExCel arena, Jijini London.

Bondia huyo wa Manchester, Fury, ambaye alimzidi pinti Chisora mwaka 2011, alibadili staili ya kupigana katika raundi ya pili na kumudu kutawala kila dakika ya mchezo huo katika kila raundi.

Bondia Chisora ambaye makazi yake yapo London, katika mchezo huo alionekana kabisa kushindwa kuonyesha makali yake, na pia kushindwa kudhibiti makombora ya mpinzani wake Tyson Fury.

Kwa ushindi huo Fury anajipanga kupigana na bingwa anayeshikilia mikanda ya uzito wa juu ya WBA, IBF na WBO mrusi Wladimir Klitschko. 
                                        Tyson Fury akimpa uppercut bondia Dereck Chisora
                    Bondia Dereck Chisora hoi akipatiwa tiba katika jeraha alilopata
   Refa wa pambano hilo akitoa ishara ya kumaliza pambano katika raundi ya kumi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni