.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 30 Novemba 2014

POLISI KENYA WAMSHIKILIA MUINGEREZA KWA KUHUSIKA NA KIFO CHA MPENZI WAKE

Polisi nchini Kenya inamshikilia mwanaume mmoja raia wa Uingereza kwa kuhusika na kifo cha mpenzi wake mwenye maradhi ya kisukari, baada ya kuziflashi chooni dawa zake katika nyumba wanaoishi iliyopo Gachie, Jijini Nairobi.

Kwa mujibu wa polisi Muingereza huyo Carl Cary Singleton mwenye umri wa miaka 41, aliteketeza dawa za mchumba wake huyo raia wa Kenya, na kumzuia ndani ya nyumba hiyo kwa siku mbili baada ya kumpiga.

Vyombo vya habari vya Uingereza vimesema Singleton walijuana kwa mara ya kwanza na mpenzi wake huyo Peris Ashley Agumbi Mumtah aliyekuwa anasoma Chuo Kikuu cha Nairobi kampasi ya Lower Kabete kwa njia ya mawasiliano ya Facebook.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni