Jumapili, 30 Novemba 2014
KOCHA WA MANCHESTER UNITED ASIFIA KIWANGO KILICHOONYESHWA JANA NA TIMU YAKE
Kocha wa Manchester United, Louis van Gaal amesema anahisi ushindi wa jana wa mabao 3-0 dhidi ya Hull City umetokana na kiwango kizuri cha uchezaji kilichoonyeshwa kwa mara ya kwanza na wachezaji wake katika msimu huu.
Katika mchezo huo Manchester United ilimiliki mpira kwa asilimia 76, wakati wakipata ushindi wao wa tatu mfululizo katika Ligi Kuu ya Uingereza, na kukaa katika nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo.
Pia kocha Louis van Gaal ameonyesha kufurahishwa na kitendo cha mchezaji Van Persie kufunga goli katika mchezo huo, hata hivyo Manchester United imejikuta ikipata pigo baada ya Angel Di Maria kuumia.
Nayo Chelsea imejikuta ikibanwa ugenini sare ya 0-0 na Sunderland huku mshambuliaji wake nyota Diego Costa akinusurika kulambwa kadi nyekudu kutokana na kucheza faulu kadhaa za kupiga kiwiko wenzake pamoja na kumpiga teke la shingo mmoja wa wachezaji wa Sunderland.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni