.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 26 Novemba 2014

UJUMBE WA WAWEKEZAJI KUTOKA UBELGIJI WATEMBELEA NHC

Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Diodorus Kamala aliyeongoza jopo la wadau wa sekta ya usafirishaji na wafanyabiashara waliotembelea nchini kuanzia Novemba 22- 29 akizungumza kwenye Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) leo asubuhi, kulia kwake ni Meneja wa Kampuni ya Ujenzi ya BS Solutions. Jopo hilo liko nchini kuangalia fursa za uwekezaji nchini. Ujumbe huo ulitoa mada kuhusu ujenzi wa nyumba kwa kutumia teknolojia rahisi ya kuunganisha na mabati maalumu ambao hutumia muda mfupi na kuwa nafuu kwa gharama. Picha zote za NHC.
Baadhi ya wadau wa sekta ya usafirishaji na wafanyabiashara waliotembelea nchini wakifuatilia kwa karibu mjadala. Jopo hilo liko nchini kuangalia fursa za uwekezaji nchini.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Jamii wa NHC, Susan Omari (kulia), Akifuatiwa na Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa NHC, Haikamen Mlekio na Mhandisi Mwandamizi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Morgan Nyonyi wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa yaiendelea katika mkutano huo.
Meneja wa Kampuni ya Ujenzi ya BS Solutions, Ing Jean Noel Galasse akifafanua jambo kwenye Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) leo asubuhi, kulia kwake ni Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Diodorus Kamala.
Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Diodorus Kamala aliyeongoza jopo la wadau wa sekta ya usafirishaji na wafanyabiashara waliotembelea nchini kuanzia Novemba 22- 29 akishukuru kabka ya ujumbe huo kuondoka kuelekea na ziara nyingine leo asubuhi.
Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Diodorus Kamala aliyeongoza jopo la wadau wa sekta ya usafirishaji na wafanyabiashara waliotembelea nchini kuanzia Novemba 22- 29 akiondoka katika chumba cha mikutano.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni