Inaonekana uhusiano wa Chris Rock na
mkewe Malaak Compton, unachukua sura ya uhasama baada ya mcheleshaji
huyo kudai katika nyaraka za kisheria alizowasilisha wiki iliyopita
kuwa mkewe anamzuia kuwaona mabinti zake kila mara.
Katika nyaraka za talaka ambazo
zimenaswa na TMZ, Chris anaomba haki ya kisheria ya kukaa na watoto
wake hao wa kike wawili Lola mwenye miaka 12 na Zahra mwenye umri wa
miaka 10.
Chris Rock na mkewe Malaak
walitangaza siku ya jumapili uamuzi wa kuvunja ndoa yao iliyodumu
miaka 20.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni