TIMU ya Coastal Union “Wagosi wa Kaya”wanatarajia kusafiriki kuelekea
nchini Kenya kesho kucheza mechi ya Kirafiki na Mombasa Combaini ikiwani sehemu ya maandalizi ya kuelekea Michuano ya Ligi kuu soka Tanzania
bara.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa soka Manispaa ya
Mombasa ambao unaatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kutokana na joto
lililopo mjini Mombasa kuelekea mechi hiyo.
Akizungumza leo, Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar Assenga amesema
maandalizi ya mechi hiyo yamekamilika kwa asilimia kubwa na kinachosu
biriwa ni siku ya mechi hiyo ambayo ni kesho.
Assenga amesema kuwa mechi hiyo itakuwa ni kipimo tosha kwa Kocha Mpya
wa timu hiyo,James Nandwa kuangalia kiwango cha timu hiyo kabla ya
kuwavaa wapinzani wao Tanzania Prison.
Hata hiyo amesema kuwa licha ya kocha huyo kuangalia kiwango cha
wachezaji ambapo mechi hiyo itakuwa ni ya pili kusimama kwenye bechi
ya kwanza ilikuwa ni kati ya Coastal Union dhidi ya Mwadui ya
shinyanga.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni