.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 5 Desemba 2014

DAKTARI WA UGANDA ALIYEPATA MAAMBUKIZI YA EBOLA NCHINI SIERRA LEONE APONA

Daktari wa Uganda aliyepata maambukizi ya Ebola nchini Sierra Leone amepona na kutoka katika hospitali aliyokuwa amelazwa nchini Ujerumani, baada ya wiki saba za matibabu katika hospitali hiyo huko Frankfurt.

Daktari huyo aliyeajiriwa na taasisi ya misaada ya Italia, alikuwa amelazwa Oktoba 3, katika kitengo cha pekee cha magonjwa ya kuambukizwa cha Hospitali ya Chuo kikuu cha Frankfurt, na aliruhusiwa Novemba 19.

Daktari huyo alikuwa amepata tatizo la viungo vyake kadhaa vya mwili kushindwa kufanyakazi, na alikuwa anahitaji kubadilishiwa viungo vya mwili, na sasa amepona na kuungana na familia yake.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni