Rais Robert Mugabe ameonyesha hasira
zake dhidi ya Makamu wa Rais wake Joyce Mujuru akidai kuwa alikuwa
akipanga njama za kumuua na kumtuhumu kuwa ni mwizi.
Akiongea katika mkutano wa chama
tawala cha Zanu-PF, Rais Mugabe amesema atawachukulia hatua maafisa
wote wala rushwa.
Rais Mugabe amesema kutokuwepo Bi.
Mujuru katika mkutano huo ni dalali za kuwa makamu wake huyo
anaogopa.
Hivi karibuni mjumbe wa Zanu-PF
aliyetimuliwa Rugare Gumbo, alidai kuwa Rais Mugabe amekigeuza chama
hicho kuwa mali yake binafsi.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni