Idara ya Sheria ya Marekani
imeanzisha uchunguzi kuhusiana na kifo cha mtu mweusi Eric Graner,
aliyekabwa koo na polisi mzungu Jijini New York.
Uchunguzi huo umetangazwa na
Mwanasheria Mkuu Eric Holder baada ya mahakama kuamua kutomfungulia
mashtaka polisi huyo.
Kundi kubwa la watu limekusanyika
Jijini New York kupinga uamuzi huo wa mahakama ya juu.
Rais Barack Obama amesema tukio hilo
linatoa picha halisi kuhusiana na namna kundi la watu wachache,
linavyoshughulikiwa na vyombo vya usimamizi wa sheria.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni